Friday 17 October 2014

BALOZI WA NORWAY AYATAKA MASHIRIKA YASIYO YA KISERIKALI KUTIMIZA MAJUKUMU YAO ILI KUAFIKIA DEMOKRASIA



Balozi wa Norway humu nchini Victor Renneberg ameyataka mashirika ya kijamii Pwani kuhakikisha yanatekeleza majukumu yao vilivyo ili kuafikia demokrasia nchini.

Akiongea kwenye kikao na wanhabari katika ofisi za shirika la Haki Afrika Renneberg amesema kuwa anatarajia kukutana na vikundi vya vijana nchini ili kujali na kuzungumzia changamoto zinazowakabili

Kwa upande wake mwenyekiti wa Haki Afrika Hussein Khalid amesema kuwa anatarajia ushirikiano mwema baina ya Kenya na Norway ambapo pia ameyataka mataifa mengine ya kigeni kutalii eneo hili ili kujionea hali ilivyo.

Renneberg na kikosi chake anatarajiwa kukutana na gavana wa Mombasa Ali Hassan na seneta Hassan Omar hii leo kabla ya kukutana na maafisa wakuu wa polisi katika kaunti ya Mombasa.

No comments:

Post a Comment

COMMENT