Wednesday 5 November 2014

UKEKETAJI WA WASICHANA WADORORESHA ELIMU LAMU


Ukeketaji wa wasichana unaoendelea kutekelezwa kila uchao katika jamii ya Boni kaunti ya Lamu umetajwa kama changamoto kuu inayosababisha kudorora kwa viwango vya elimu katika eneo hilo.
 
Haya ni kwa mujibu wa afisa mkuu wa elimu ya afya,jinsia na jamii katika kaunti hiyo Hamisi Kaviha ambapo amesema hali hiyo inaendelea kuzidi na kusababisha wasichana wengi kupachikwa mimba miongoni mwao 15 kutoka shule ya msingi ya Bargoni.

Akizungumza na wanahabari wakati wa ziara yake katika eneo la Boni Kaviha ameeleza kuwa afisi yake ilibaini kwamba shughuli hiyo hutekelezwa kwa watoto walio kati ya umri wa miaka 9 na 10 hasa kwenye sherehe za mwezi December.

Amedokeza kuwa baada ya wasichana hao kukeketwa wao hujihisi kwamba wako katika nafasi ya kupata kuolewa mapema kabla ya umri wao kufika.

Hata hivyo amesema wameweka mikakati ya kushirikiana na machifu pamoja na viongozi wengine ili kuwakamata wale ambao wanahusika na maafa hayo.