Wednesday 16 April 2014

THAMANI YA KIFO: MTOTO ALIYETAFUNWA NA MBWA AFIDIWA LAKI MOJA KILIFI


Familia iliyopoteza mtoto wa mwaka mmoja baada ya mtoto huyo kuvamiwa na  kutafunwa na mbwa, imelipwa fidia ya shilling laki moja.
Kulingana na ripoti ya gazeti la “Daily Nation” fidia hiyo iliafikiwa baada ya mwenye mbwa huyo, Bwana Mohamed Hajj Awadh, ambaye pia nimwenye shamba la “kilifi’s shariani poultry farm”, kujadiliana na wazazi wa mwendazake.
Mtoto huyo alivamiwa pale alipokuwa akitambaa kumfuata babake aliyekuwa akielekea shambani mwa bwana Mohamed anamo fanya kazi kama kibarua.
Alipokuwa akithibitisha kupokea kwa fidia hiyo, baba ya mtoto huyo, Mwampa kadodo, mwenye umri wa miaka 27, alisema kwamba yeye na mkewe walitaka kuendeleza uhusiano mwema na mwajiri wake.
Ijapo kuwa uchungu wa kumpoteza mwana ulikuwa mwingi, ametambua kwamba  hakuna anachoweza kukifanya ili kumrudishia mwanawe uhai.
“ Ni uchungu ndio lakini kwa upande mwingine huu ulikuwa mpango wa mungu ambao hatuna nguvu kuuliko. Uhusiano wetu na mwajiri wangu bado ni mzuri nab ado nafanya kazi shambani mwake.”
Mwenye shamba pia alikuwa na huzuni moyoni kuhususiana na kisa chote.
“ilikuwa jambo la kushtua na kuhuzunisha,” alisema.
Bwana Kadodo, baba ya watoto watano, wavulana watatu na wasichana wawili alisema kwamba atatumia fidia hiyo kuwasomeshea watoto wake walio na umri kati ya mmoja na sita.
“Msichana wangu wa kwanza yuko darasa la kwanza kama mdogo wake. Nitazitumia pesa hizi kulipia karo yao. Hawa wengine watatu bado wako nyumbani,” Alisema.
Mapatano hayo yaliiafikiwa chini ya uelekezi wa afisaa kutoka kwa shirika la haki za kibinadamu, Eric Mgoja. Mgoja alizisifu pande zote mbili kwa hatua walioichukua ili kuona kwamba utata baina yao umetatuliwa.
Hata hivyo mama ya mtoto  huyo amelihama shamba hilo kutokana na majeraha  ya kisaikolojia.

No comments:

Post a Comment

COMMENT