Tuesday 18 November 2014

WATU 600 WAWEKWA KARANTINI KWA HOFU YA MAMBUKIZI MALI


Nchini Mali, watu 600 wako chini ya uchunguzi wa maambukizi ya Ebola wakati huu nchi hiyo ya Afrika Magharibi ikiweka mikakati kuzuia maambukizi mapya ya ugonjwa huo hatari.
 
Wakati hayo yajikiri, viongozi wa serikali walikutana Jumatatu Novemba 17 kuweka mikakati ya kuhakikisha kuwa usalama unaimarishwa hasa katika mpaka wake na Guinea, nchi iliyoathiriwa zaidi na ugonjwa wa Ebola.

Hadi sasa watu wawili wamepoteza maisha nchini Mali baada ya kuambukizwa Ebola.
Rais Ibrahim Boubacar Keita, amezuru katika mpaka wa nchi hiyo na Guinea katika eneo la Kouremale na kutoa wito kwa wenyeji kuhakikisha kuwa wanasaidia kupambana na ugonjwa huu kwa kutoa ripoti kwa yeyote anayeshukiwa kuambukizwa.

Umoja wa Ulaya umeahidi kutoa Dola Milioni 15 kwa nchi ya Mali, Senegal na Cote d'Ivoire ili kuweka mikakti ya kuzuia kusambaa kwa Ebola kutoka nchi jirani kama Guinea, Liberia na Siera Leone.

Shirika la afya duniani, limesema zaidi ya watu elfu tano wamepoteza maisha katika nchi za Afrika Magharibi kutokana na ugonjwa wa Ebola.

No comments:

Post a Comment

COMMENT